Mechi ya Nani Mtani Jembe namba 2 itafanyika kesho siku ya jumamosi katika dimba la Uwanja ambapo itawakutanisha Young Africans Sports Club dhidi ya Simba SC huku timu  zote zikitarajiwa kuwatumia wachezai wao wapya zilizowasajili katika kipindi cha dirisha dogo.
Kikosi cha mbrazil Marcio Maximo tayari kimeshawasajili wachezaji wawili kiungo Emerson de Oliveira kutoka nchini Brazil na mshambuliaji mkongwe na mzoefu wa hali ya juu Danny Mrwanda ambao wanatajiwa kuongeza nguvu katika mchezo huo wa kesho.
Young Africans chini ya kocha mkuu Marcio Maximo inaendelea na mazoezi katika Uwanja wa Boko Veterani  huku wachezaji wote 26 waliongia kambini wakiendelea kujifua kuwa fit kwa ajili ya mchezo huo wa siku ya jumamosi.
Huu ni mchezo wa pili wa Nani Mtani Jembe kuzikutanisha timu hizi kwani katika mchezo wa awali uliofanyika mwaka jana, Young Africans ilipoteza kwa mabao 3- 1, na kocha Maximo pamoja na wachezaji wake wamejiandaa kuhakikisha safari hii wanapata ushindi kwenye mchezo huo.

Kocha Maximo amesema vijana wake wote wapo kwenye hali nzuri kuelekea mchezo huo, ambapo mchezaji pekee majeruhi ni Jerson Tegete ambaye alipata majeraha hayo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Vipers kutoka nchini Uganda.

Advertisement

 
Top