Bondia nyota zaidi nchini, Francis Cheka ameachiwa huru.
Cheka ameachiwa huru baada ya kushinda rufaa yake aliyokata kupinga kifungo cha miaka mitatu gerezani.
Tayari Cheka alianza kutumikia kifungo hicho mjini Morogoro.
Lakini taarifa za uhakika zinasema ameachiwa leo baada ya kushinda rufaa hiyo.
“Tayari ameachiwa, lakini tunashughulikia masuala kadhaa kumalizia ishu hiyo. Ila tayari yuko nje,” alisema Kaike Siraju, promota wa ngumi za kulipwa aliyekuwa akipambana kuhakikisha Cheka anatoka.