Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic amesisitiza
hata kama iko ugenini, Simba inalazimisha kushinda dhidi ya Kagera Sugar.
Kocha huyo Mserbia amesema mechi hiyo ya
wikiendi itakuwa ngumu kwao kutokana na ubora, lakini suala la ushindi ni
muhimu.
“Ila kuna timu kongwe na timu imara zaidi. Sisi tunachoangalia
ni kufanya vizuri na kushinda.
“Tutaanza safari ya kwenda Kagera tukiwa na
lengo moja tu, kushinda mechi na kurudi na pointi tatu,” alisisitiza MSerbia huyo.