Mabondia Mohammed Matumla, kutoka Tanzania pamoja na Wang Xin Hua ambaye ni raia wa China, jana mchana  wamepima uzito tayari kwa mhezo wao wa kimataifa wa Masumbwi utakao pigwa katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo
Wapiganaji hao kila mmoja ametoa tambo zake pamoja na vitisho kwa mwenzake, ambapo Matumla ametamba kuwa ni lazima  amzimishe mpinzani wake huyo kutoka China, nae Hua akafunguka  na kusema haitakuwa lahisi na anachoamini Matumla atamkalisha kwa KO.
Mohammed amekuwa akinolewa baba yake mzazi Rashid Matumla ambaye alikuwa bondia mahiri na aliyeshinda mataji mawili ya dunia kwa nyakati tofauti.
Mbali na mabondia hao pia Bondia Mada Maugo atapanda ulingoni kuzichapa na mpinzani wake Japhet Kaseba, ambapo Wawili hao watapambana katika pambano la utangulizi kabla ya Mohammed Matumla hajapanda ulingoni kumvaa Mchina.


Add caption

Advertisement

 
Top