Kwanza nianze kwa
kuwapongeza Yanga s.c kwa kazi waliyoifanya katika mechi dhidi ya Etou
du Sahel, nimeanza kuwapongeza Yanga kwa sababu ya uwezo ulioneshwa na
Etou du Sahel, kiufupi naamini kila mmoja atakuwa na mtazamo wake kuhusu
mechi hiyo, kuna watu wanasema kukosekana kwa Salum Telela lilikuwa
pengo kubwa na wengine wanasema yao pia.
Lakini kikubwa ni
kuifanyia tathmini mechi yenyewe, wakati kabla haijaanza tulikuwa
tumekaa pamoja na Emmanuel Arnold Okwi, ikaletwa listi ya vikosi
vitakavyoanza na wachezaji wa akiba, mmoja kati ya wachezaji ambao
aliwaonesha kuwa ni hatari ni anayevaa jezi namba 12 ambaye ni Franck
Kom, akasema kuwa alimuacha wakati anaondoka Etou du Sahel, na
tulilithibitisha hilo baada ya mpira kuanza, jamaa alitawala ile mbaya
sehemu ya kiungo, alikuwa anafanya anachotaka, ana nguvu, ana kasi, na
mpira anaujua.
Najiuliza hata
angekuwepo Salum Telela je angeweza kupambana na huyu mtu ambaye
anacheza easy game huku akitumia nguvu panapostahili.
Tukiangalia pia timu
nzima ya Etou du Sahel kiujumla walikuwa vizuri sana kuliko Yanga,
walitawala mchezo, walijiamini, walitumia ukubwa wa miili yao kufanya
blocking, walitumia vizuri vimo vyao katika mipira ya vichwa, hili
liliwafanya Yanga wapoteze mipira Mingi na kutoka mchezoni kipindi cha
kwanza, lakini hata kipindi cha pili baada ya waarabu kurudisha goli
Yanga walijaribu ku
tulia ili wapate bao la ushindi lakini bado mambo yalikuwa magumu mno.
tulia ili wapate bao la ushindi lakini bado mambo yalikuwa magumu mno.
Nachokusudia hapa ni
kwamba kumekuwa na kasumba ya watanzania kulalamika siku zote kuwa
tukienda kucheza na waarabu tunaonewa, mimi pia nakubaliana na fact
hiyo, lakini bado nina wasiwasi na uwezo wa timu zetu, tumeshashuhudia
mechi nyingi ambazo waarabu wamekuja kucheza hapa, tunajiona kabisa kuwa
uwezo wetu kwa hawa jamaa tupo chini, mfano mzuri ni mechi ya jana tu,
kila mtu ameona jinsi waarabu wameonesha wamelelewa kisoka, wamafanya
wanachokitaka, na uwezo wa mchezaji mmoja mmoja walikuwa wako juu.
Tuangalie pia hata timu
yao ya taifa ya Tunisia imeshiriki kombe la mataifa ya Afrika mara
ngapi na sisi tumeshiriki mara ngapi?, ubora wa ligi yao ndio umewafanya
washiriki mara nyingi kombe la mataifa ya Afrika, lakini bado tunataka
kuamini vilabu vyetu ni bora kuliko wao, hivi ni kweli?
Ukitazama hata
mazingira ya timu, mishahara ya wachezaji wao ipo juu. Mpira unahitaji
uwekezaji na sio blaa blaa tu. Mpira ni mchezo wa wazi hauchezwi
chumbani, unachezwa uwanjani kila mtu anaona, tuache utamaduni wa
kusifiana ujinga, tuhamasishane kuwekeza katika soka na kuwa na malengo
ya mbali .
Etou du Sahel
wametuumbua kwa kuonesha kuwa soka lao lipo juu, na walilazimisha
matokeo ya mechi. Tusubiri mechi ya Marudiano pengine Yanga watanifanya
nionekane muongo katika uchambuzi wangu kwa kuwatoa waarabu.