Wachezaji wa Azam FC wakishangilia goli lililofungwa na John Bocco 'Adebayor'
Wachezaji wa Azam FC wakishangilia goli lililofungwa na John Bocco ‘Adebayor’
John Bocco ‘Adebayo’ na Kipre Tchetche wameipeleka Azam kwenye hatua ya robo fainali baada ya kila mmoja kufunga goli kwenye mchezo wa leo kati ya Azam FC dhidi ya Malakia ya Sudan Kusini ikiwa ni mwendelezo wa michuano ya Kagame Cup ambapo Azam ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-0.
Bocco alianza kuifungia Azam goli la kuongoza dakika ya 27 kipindi cha kwanza kwa mpira wa adhabu ndogo nje kidogo ya eneo la hatari la Malakia goli lililoipeleka Azam mapumziko ikiwa mbele kwa goli 1-0.
Azam vs Malakia 7Kipindi cha pili kocha wa Azam FC Stewart Hall alifanya mabadiliko kwa kumtoa Ame Ali ‘Zungu’ na nafasi yake kuchukuliwa na Kipre Tcheche ambaye alifunga goli la pili dakika ya 52 ya kipindi cha pili. Gadiel  Michael alipumzishwa kumpisha Shah Farid Mussa wakati Abbas Mudathir Yahya aliingia kuchukua nafasi ya Salum Abubakari ‘Sure Boy’.
Azam walitawala sehemu kubwa ya mchezo huo  huku mchezaji wao mpya Jean Mugiraneza waliemsajili kutoka APR FC  ya Ruanda akionekana kuimudu vyema nafasi ya kiungo wa ulinzi hali iliyosababisha punguza mashambulizi ya mara kwa mara kwenye lango la Azam.
Azam vs Malakia 5Pascal Wawa ametangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo wa leo (man of the match) na kuzawadiwa king’amuzi na kituo cha DSTV.
Mchezo wa awali uliopigwa saa nane mchana kwenye uwanja wa taifa kati ya Al Shandy (Sudan) dhidi ya LLBA FC (Burundi) ulimalizika kwa sare ya kufungana goli 2-2.
Kikosi cha Azam kilichoanza: Aishi Mnula, John Bocco ‘Adebayor’, Pascal Wawa, Agrey Morris, Shomari Kapombe,  Salumu Abubakar,  Frank Domayo, Ame Ali, Jean Mugiraneza,  Kamagi Gadiel Michael,  Kheri Abdallah Salum
Azam vs Malakia 2Walioanzia kwenye benchi: Mwadini Ali,  Kipere Tchetche, Mudathir Yahya, Shah Farid Mussa, Erasto Nyoni, Morad Said Husein, Himid Mao , Didier Kavumbagu na Metacha Boniface Mnata

Advertisement

 
Top