Nahodha wa Azam FC John Bocco (kulia) akikabidhiwa kombe la Kagame na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadick na Raila Odinga baada ya mchezo wa fainali walioshinda kwa goli 2-0 dhidi ya Gor Mahia
Nahodha wa Azam FC John Bocco (kulia) akikabidhiwa kombe la Kagame na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadick na Raila Odinga baada ya mchezo wa fainali walioshinda kwa goli 2-0 dhidi ya Gor Mahia
Azam wametangazwa kuwa mabingwa wapya wa kombe la Kagame lilinaloshirikisha vilabu bingwa vya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati baada ya kuibwaga timu ya Gor Mahia ya Kenya kwa goli 2-0 kwenye mchezo wa fainali uliopigwa leo jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Azam yamezamishwa wavuni na John Bocco aliyefunga goli la kwanza na Kipre Tchetche akamaliza matumaini ya Gor Mahia kutwaa taji hilo kwa mara ya tano baada ya kuifungia Azam goli la pili na la ushindi kwenye mchezo wa leo.
Azam Kagame 2Ubingwa huo wa kombe la Kagame ni wa kwanza kwenye historia ya Azam baada ya kuingia kwenye fainali mara mbili. Fainali ya kwanza walicheza mwaka 2012 dhidi ya Yanga na kupoteza kwa goli 2-0 na mwaka huu (2015) wameweka rekodi ya kulinyakua kombe hilo bila kuruhusu kufungwa goli.
Azam FC walipata goli la kwanza dakika ya 16 kipindi cha kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao John Bocco akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Kipre Tchetche aliyewatoka walinzi wa Gor Mahia kisha kuachia krosi iliyomkuta Bocco ndani ya boksi la Gor Mahia na kuupachika mpira wavuni kuiandikia Azam goli la kuongoza
Azam KagameKipindi cha kwanza kilimalizika Azam wakiwa mbele kwa goli 1-0 dhidi ya Gor Mahia goli lililowekwa kambani na John Bocco ‘Adebayor’.
Kipindi cha pili kilipoanza, Azam walifanya mabadiliko kwa kumtoa Shah Farid Mussa na kumuingiza Erasto Nyoni
Daika ya 50 kipindi cha pili Azam FC walifanya shambulizi kali ambapo Kipre Tchetche aliwatoka mabeki wa Gor Mahia na kuachia shuti kali lililogonga mwamba wa pembeni na kutoka njeya uwanja.
Azam Kagame 6Kipre Tcheche akaifungia Azam goli la pili dakika ya 64 kwa mpira wa adhabu ndogo alioupiga nje kidogo ya 18 ya goli la Gor Mahia baada ya Shomari Kapombe kuangushwa na Aucho Khalid. Mpira uliopigwa na Tchetche ulienda moja kwa moja wavuni bila ya mlinda mlango Boniface Oluochi kuona uliko pitia.
Azam walifanya mabadiliko tena ambapo dakika ya 68 walimtoa Ame Ally ‘Zungu’ akaingia Frank Domayo na dakika ya 88 Kipre Tchetche akapumzishwa kumpisha Didier Kavumbagu.
Azam Kagame 7Wachezaji wa Gor Mahia walionekana kuchanganywa na goli la pili kwani walikuwa wakiwafanyia madhambi wachezaji wa Azam na mara nyingingi walionekana kutoridhishwa na maamuzi ya Louis Hakzimana wa Rwanda ambaye alichezesha mhezo huo. Wachezaji kadhaa wa Gor Mahia walioneshwa kadi ya njano kwa mchezo wao mbaya.

Advertisement

 
Top