Kipa Juma Kaseja amesaini mkataba wa miezi sita kuitumikia Mbeya City.
Kaseja amesaini mkataba huo leo rasmi mbele ya meneja wake mpya, Athumani Tippo pamoja uongozi wa Mbeya City.
Shughuli hiyo ya kusaini imefanyika jijini Dar es Salaam muda mchache uliopita.
Kaseja anajiunga na Mbeya City baada ya kuwa ameitumikia Yanga ambayo hata hivyo hawakuwezana mwishoni.

