![]() |
raisi tff:jamar malinzi |
Rais wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini – TFF Bw. Jamal Malinzi ametuma salamu za
pongezi kwa Wenyekiti wa klabu ya African Sports (Tanga) , Majimaji
(Ruvuma), Mwadui (Shinyanga) na Toto Africans ya Mwanza kwa timu zao
kupanda Ligi Kuu ya Vodacom (VPL).
Katika
salamu zake Bw. Malinzi amesema vilabu hivyo vinapaswa kujipanga na kufanya
maandalizi kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom 2015/2016, kwani VPL
ni ngumu kutokana na timu zote kuwa na ushindani mkubwa wa kutafuta matokeo
mazuri kuepeuka kushuka daraja.