Hatimaye
Simba sasa imekuwa na uhakika wa kumbakiza kiungo wake mbunifu, Awadh
Juma baada ya kukubaliana kumwongezea mkataba wa miezi 18.
Awadh,
mchezaji wa zamani wa Mtibwa Sugar, amekuwa akikubalika kwa kocha wake,
Dylan Kerr ambaye mara kadhaa amekuwa akikiri kumkubali mchezaji huyo
kiasi cha kukiri kuwa ndiye anayesaidia kuunganisha safu ya kiungo na
ushambuliaji kikosini kwake.
Awadh
alisema kuwa alimalizana na viongozi wa timu hiyo jana Alhamisi kwa
kukubaliana kuongeza mkataba wa muda huo, ada ya usajili na mambo
mengine ndani ya mkataba na kwamba kilichobaki sasa ni makabidhiano
kisha yeye amwage wino.
“Tumemalizana,
tumeshaelewana juu ya kila kitu kwamba nitaongeza mwaka na nusu, dau la
usajili na mambo mengine, kwa hiyo bado kusaini ambapo natarajia zoezi
hilo litakamilika ndani ya siku mbili hizi kabla ya mechi yetu na Azam
FC,” alisema Awadh anayefananishwa na mchezaji wa zamani wa Ureno,
Maniche.